Rais Donald Trump wa Marekani amekubali ombi la Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un la kutaka wakutane mapema ndani ya mwezi Mei mwaka huu,na hivyo kuweka historia kufuatia kutokuwepo rais wa Marekani ambaye amewahi kuonana na kiongozi mkuu wa Korea kaskazini.
JENGO la ofisi ya serikali ya mtaa katika eneo la Goba jijini Dar es Salaam ambalo hutumiwa na polisi, limeangukiwa na mnara wa simu kutokana na mvua iliyonyesha juzi usiku na kumjeruhi askari.